• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 3:09 PM
Barcelona walazimishiwa sare ya 3-3 dhidi ya Celta Vigo

Barcelona walazimishiwa sare ya 3-3 dhidi ya Celta Vigo

Na MASHIRIKA

BARCELONA walitupa uongozi wa 3-0 dhidi ya Celta Vigo katika mchuano wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) ulioshuhudia wakilazimishiwa sare ya 3-3 ugenini.

Mechi hiyo ilikuwa ya mwisho ya kocha mshikilizi Sergi Barjuan kusimamia katika kikosi cha Barcelona ambacho kitakachokuwa chini ya mkufunzi Xavi Hernandez kuanzia Novemba 8, 2021.

Mabao kutoka kwa Ansu Fati, Sergio Busquets na Memphis Depay yaliweka Barcelona katika uongozi wa 3-0 kufikia dakika ya 34.

Hata hivyo, Iago Aspas alicheka na nyavu za Barcelona mara mbili, ikiwemo kusawazisha mambo katika dakika ya 96, na kusaidia Celta Vigo kurejea mchezoni kwa matao ya juu.

Nolito alifanya mambo kuwa 3-2 zikisalia dakika 16 pekee kwa mchezo kukamilika huku bao la pili la Aspas likimaanisha kwamba Barcelona kwa sasa wamesakata jumla ya michuano minne bila kushinda wowote katika La Liga.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Handiboli: Midume wa chuo Kikuu cha Kenyatta wafuzu gozi la...

Neymar na Mbappe wabeba PSG dhidi ya Bordeaux ligini

T L