• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:55 AM
Beki Calum Chambers aondoka Arsenal na kutua Aston Villa

Beki Calum Chambers aondoka Arsenal na kutua Aston Villa

Na MASHIRIKA

ASTON Villa wamemsajili beki Calum Chambers kutoka Arsenal kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 ana uwezo wa kuwajibishwa kama beki wa kulia au beki wa kati. Kibarua chake cha kwanza kambini mwa Villa ni mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) dhidi ya Leeds United mnamo Februari 9, 2022 ugani Villa Park.

Chambers alijiunga na Arsenal mnamo 2014 baada ya kuagana na Southampton. Amewajibishwa na timu ya taifa ya Uingereza mara tatu tangu wakati huo. Amechezea Arsenal mara 122 katika mashindano yote na akasaidia kikosi hicho kushinda taji la Community Shield na Kombe la FA katika kipindi hicho.

Akiwa Arsenal, aliwahi kutumwa kambini mwa Fulham na Middlesbrough kwa mkopo. Kocha Mikel Arteta wa Arsenal amemchezesha mara tano pekee msimu huu wa 2021-22.

Chambers anakuwa mchezaji wa nne baada ya Philippe Coutinho, Lucas Digne na Robin Olsen kusajiliwa na kocha Steven Gerrard wa Villa mwezi huu.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Kocha wa DCI anapongeza vipusa wake kwa kujituma mazoezini

TUSIJE TUKASAHAU: Wakongwe waliopewa kadi za NHIF...

T L