• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 3:09 PM
Beki Ronald Araujo sasa kuchezea Barcelona hadi 2026

Beki Ronald Araujo sasa kuchezea Barcelona hadi 2026

Na MASHIRIKA

BEKI Ronald Araujo amerefusha mkataba wake kambini mwa Barcelona hadi mwaka wa 2026 huku kikosi kitakachohitaji huduma zake kuanzia sasa hadi wakati huo akilazimika kuweka mezani Sh131 bilioni.

Kandarasi ya awali kati ya nyota huyo raia wa Uruguay na Barcelona ilitarajiwa kutamatika mwishoni mwa mwaka 2023.

Araujo, 23, amechezea Barcelona mara 26 katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) msimu huu huku akifunga mabao manne, likiwemo moja katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Real Madrid katika mkondo wa pili wa gozi kali la El Clasico.

Araujo alijiunga na Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano mnamo 2018 baada ya kuagana rasmi na klabu ya Boston River nchini Uruguay.

Mnamo 2019, alitokea benchi na kuchezea Barcelona kwa mara ya kwanza dhidi ya Sevilla ila akatimuliwa uwanjani baada ya dakika 14 pekee kwa kosa la kumchezea visivyo Javier Hernandez.

Amechezea Uruguay mara tisa tangu awajibishwe kwa mara ya kwanza ndani ya jezi za timu ya taifa mnamo 2020.

  • Tags

You can share this post!

Urusi yatishia kuzusha Vita vya Tatu vya Dunia iwapo...

Nassir adai Kalonzo ana nia fiche dhidi ya Odinga

T L