Na JOHN KIMWERE
BEKI wa Kibera Black Stars FC (KBS), Nicodemus Onyango anaamini kuwa wanatosha mboga kufanya kweli kwenye ngarambe ya Supa Ligi ya Taifa (NSL) na kutwaa tiketi ya kushiriki Ligi Kuu Kenya (FKF-PL) muhula ujao.
Mpiga gozi huyu ambaye ni mara ya tatu anachezea timu hiyo amepania kuisadia kunasa tiketi ya kupandishwa ngazi kama alivyochochea FC Talanta kufuzu kushiriki Ligi Kuu Kenya.
”Tumeshiriki NSL kwa muda mrefu sasa ni vizuri nasi tujitume kiume kupigania nafasi ya kupanda ngazi,” anasema na kuongeza kuwa ana imani mchango wake utasaidia kikosi hicho.
Anashikilia kuwa baada ya kutazama kikosi hicho kwa umakini amegundua wanakaa vizuri kumaliza kati ya nafasi mbili bora katika jedwali.
Anashauri wenzake kuwa wakaze buti buti kwenye mechi zao ili kutimiza azma yao maana muhula huu wameanza vyema. Difenda huyu aliyewahi kupigia wana benki wa KCB FC ya FKF-PL, msimu uliyopita alikuwa akisakatia FC Talanta.
KBS FC