• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Blackburn Rovers wapata kocha mpya

Blackburn Rovers wapata kocha mpya

Na MASHIRIKA

BLACKBURN Rovers wamemteua John Dahl Tomasson kuwa kocha wao mpya kwa mkataba wa miaka mitatu.

Fowadi huyo wa zamani wa Denmark, Newcastle United na AC Milan anajaza pengo la Tony Mowbray aliyebanduka kambini mwa kikosi hicho cha Ligi ya Daraja ya Kwanza nchini Uingereza (Championship) mnamo Mei 2022 baada ya kipindi cha miaka mitano.

Tomasson, 45, anajiunga na Rovers baada ya kuongoza Malmo FF kunyanyua taji la Ligi Kuu ya Uswidi kwa misimu miwili mfululizo.

Blackburn walikamilisha kampeni za Championship mnamo 2021-22 katika nafasi ya nane kwa alama nane nje ya nafasi ya kufuzu kwa mchujo wa kupandishwa ngazi hadi Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Osano analenga Tuzo ya Mnyakaji Bora muhula ujao

Ruto amkaripia Raila kufuatia vurugu zilizotokea Jacaranda

T L