• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Buffon kuagana rasmi na Juventus mwishoni mwa msimu huu

Buffon kuagana rasmi na Juventus mwishoni mwa msimu huu

Na MASHIRIKA

KIPA veterani wa Juventus, Gianluigi Buffon amesema kwamba ataondoka kambini mwa kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Italia (Serie A) mwishoni mwa msimu huu.

Buffon, 43, amejizolea jumla ya mataji 10 ya Serie A na mengine manne ya Italian Cup katika awamu mbili za kuhudumu kwake kambini mwa Juventus. Alirejea jijini Turin, Italia kuchezea Juventus mnamo 2019 baada ya kuwadakia Paris Saint-Germain (PSG) kwa kipindi cha msimu mmoja.

“Tumefika mwisho wa mzunguko na nahisi kwamba huu ndio wakati mwafaka zaidi wa kuagana na Juventus. Uhusiano huu mzuri na wa muda mrefu kati yangu na Juventus unatamatika rasmi mwishoni mwa mwaka huu,” akasema Buffon aliyewahi kushinda Kombe la Dunia akiwanyakia Italia.

“Pengine nitaacha kabisa kucheza au nifikirie upya kurejea uwanjani iwapo nitapata fursa itakayonichochea zaidi. Sitahofia kitu. Nahisi kwamba nimejitolea yangu yote kuwajibikia Juventus ambayo pia imefanya chote kilichowezekana kunifaa kitaaluma na katika kiwango cha mtu binafsi. Sidhani kuna zaidi,” akaongeza.

Buffon ambaye anajivunia kuchezea Juventus mara 176, anashikilia rekodi ya mchezaji aliyewahi kuwajibishwa katika Serie A mara nyingi zaidi (mechi 656).

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Genge laibuka upya nakujeruhi watu 7 mtaani

Sporting Lisbon washinda taji la Ligi Kuu ya Ureno kwa mara...