• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:55 AM
Bunyore Starlets waanza msimu mpya wa FKF-WPL kwa kishindo

Bunyore Starlets waanza msimu mpya wa FKF-WPL kwa kishindo

NA TOTO AREGE

WAREMBO wa Bunyore Starlets walianza msimu wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF-WPL) kwa mpigo na sasa wanaongoza katika jedwali wakiwa na alama sita kutokana na mechi mbili.

Wakiongozwa na mfungaji matata na mshindi wa Kiatu cha Dhahabu msimu wa 2022/23, Airine Madalina, walipata ushindi wa 4-0 dhidi ya Trans Nzoia Falcons katika Uwanja wa Mumboha huko Luanda, Kaunti ya Vihiga. Madalina alifunga mabao mawili kwenye mechi hiyo.

Baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Kibera Girls Soccer, mabingwa watetezi Vihiga Queens, wako katika nafasi ya pili kwenye jedwali wakiwa na alama sawa na Bunyore lakini tofauti ya magoli.

Nao Nakuru City Queens wameshikilia nafasi ya tatu na alama nne baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Zetech Sparks ambao wako kwenye nafasi ya tano.

Kwa upande mwingine, Kenya Police Bullets wamepanda hadi nafasi tatu juu baada ya ushindi wa 5-2 dhidi ya Bungoma Queens. Ulinzi Starlets nao, katika nafasi ya sita, walishinda mechi yao ya kwanza ya msimu kwa kuwanyorosha Wadadia Women 3-0.

Wageni katika ligi kuu, Soccer Assassins, bado hawajacheza mechi ya ligi na kwa sasa wako katika nafasi ya 10.

Bungoma Queens, Wadadia Women, Gaspo Women, na Kibera wako katika nafasi za saba, nane, 10, na 11 mtawalia.

  • Tags

You can share this post!

Mwanamume ashtakiwa kwa kumteka nyara mkewe

Mwanamuziki Vivian afunguka sababu za ndoa yake na Sam West...

T L