• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Mwanamuziki Vivian afunguka sababu za ndoa yake na Sam West kuingia doa

Mwanamuziki Vivian afunguka sababu za ndoa yake na Sam West kuingia doa

NA FRIDAH OKACHI

MWANAMUZIKI tajika Vivian Wambui maarufu kama Vivian amefunguka kuhusu sababu za ndoa yake na aliyekuwa mumewe, Sam West, kuvunjika.

Kulingana na msanii huyu, sababu kuu ya ndoa yake kusambaratika ni kwamba hakuwa tayari kuwa mke.

Hali kadhalika, Vivian anasema mchumba wake alikuwa na matarajio mengi ambayo hangeweza kutimiza.

Sam West ni mfanyabiashara, na mwasisi wa kituo cha redio cha Hero FM – ambacho kimefungwa na vilevile alikuwa produsa na meneja wa Vivian.

“Nilimweleza kuhusu urafiki wetu; Nikamuarifu kuhusu umuhimu wa kujuana zaidi…Nilihisi mambo mengi hayakuwa wazi na hatukuwa tumeyazungumzia,” Vivian akasema.

Mwanamuziki huyu alifunguka wakati wa mahojiano ya kipekee na Mwanakontenti Mwafreeka, kupitia Makala yake ya Iko Nini, You Tube.

Vivian alifichua kwamba wawili hao walikuwa wamekubaliana kuishi pamoja, akabadilisha nia na kuchukua mkondo mwingine.

“Waelewa sasa mbona nilitaka tuwe kwenye ukurasa mmoja?” alihoji.

Aliendelea kueleza kwamba alihisi walihitaji muda zaidi kujuana na kuelewana.

Vivian na Sam West waliweka wazi kuhusu mahusiano yao baada ya kuchumbiana kwa muda wa mwaka mmoja.

Aidha, mfanyabiashara huyo aliomba posa kuwa kwenye ndoa na Vivian kupitia runinga moja nchini 2017.

Pendekezo hilo lilipeperushwa moja kwa moja.

Hata hivyo, miaka mitano baadaye waliachana, Vivian akiainishia Sam West sababu za kutaka wavunje ndoa.

“Aliondoka akiwa mwenye hasira. Nafikiri sababu ilikuwa kukosa kutimiza matarajio yake. Alitaka niwe mtu fulani…Na alipoondoka, nilihisi nahitaji muda zaidi,” alifafanua.

Mwanamuziki huyu alilalamikia mumewe kumchunguza zaidi, na alichohitaji ni mwanamume asiye na matarajio mengi kuliko yale ambayo angeweza kutimiza.

Kwa sasa, Vivian anaendeleza taaluma yake ya uanamuziki japo yupo nje ya nchi.

  • Tags

You can share this post!

Bunyore Starlets waanza msimu mpya wa FKF-WPL kwa kishindo

Mwili wa dereva wa teksi wapatikana baada ya washukiwa...

T L