• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:55 AM
Buriram yafungua mwanya wa alama 10 Ligi Kuu ya Thailand

Buriram yafungua mwanya wa alama 10 Ligi Kuu ya Thailand

Na GEOFFREY ANENE

KLABU ya Buriram United imefungua mwanya wa alama 10 juu ya jedwali la Ligi Kuu ya Thailand baada ya kulipua Port 2-1 Jumamosi.

Buriram ilipata mabao yake kupitia kwa Jonathan Bolingi dakika ya 20 (penalti) na Supachai Chaided dakika ya 78 uwanjani Chang Arena.

Nattawut Sombatyotha alipachika bao la Port kujifariji dakika ya 87.

Mkenya Ayub Masika aliangushwa na Tanaboon Kesarat ndani ya kisanduku cha penalti na kumpa Bolingi fursa ya kuweka Buriram kifua mbele dakika ya 20. Tukio hilo lilihitaji kuangaliwa kwenye video kuthibitishwa ilikuwa penalti.

Masika alicheza dakika 72 kabla ya kupumzishwa na nafasi yake kujazwa na Suphanat Mueanta. Kufuatia ushindi huo, Buriram ilidumisha rekodi yake ya kutoshindwa na Port hadi mechi saba (ushindi tano na sare mbili).

Mchuano ujao wa Buriram ni dhidi ya Nakhon Ratchasima mnamo Februari 27. Buriram inaongoza kwa alama 48 ikifuatiwa na Bangkok United (38), Pathum United (38), Chonburi (35) na Muangthong (34) katika nafasi tano za kwanza.

  • Tags

You can share this post!

Jenerali Badi ajikuta katika kashfa ya ardhi

PAA yajitenga na ziara ya Raila Pwani

T L