• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Celtic wakung’uta AZ Alkmaar kwenye mchujo wa Europa League

Celtic wakung’uta AZ Alkmaar kwenye mchujo wa Europa League

NA BBC

UTHABITI wa Celtic chini ya Ange Postecoglou uliendelea kudhihirika usiku wa Jumatano baada ya miamba hao wa Ligi Kuu ya Scotland kupokeza AZ Alkmaar kichapo cha 2-0 katika mechi ya kufuzu kwa hatua ya makundi ya Europa League.

Kyogo Furuhashi aliwaweka Celtic kifua mbele katika dakika ya 12 baada ya kushirikiana vilivyo na Tom Rogic. Bao hilo lilikuwa lake la sita kutokana na mechi sita tangu aingie rasmi kambini mwa Celtic.

Bao la pili la Celtic lilifumwa wavuni na James Forrest aliyejifunga mwanzoni mwa kipindi cha pili. Mechi ya marudiano itasakatwa Alhamisi ijayo jijini Amsterdam.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Batshuayi arefusha mkataba wake kambini na Chelsea na kutua...

Mchujo wa UDA utaendeshwa kwa njia huru na haki, Ruto asema