• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:50 AM
Chelsea waanza kujiandaa kwa msimu mpya wa 2021-22 kwa ushindi mnono wa 6-1

Chelsea waanza kujiandaa kwa msimu mpya wa 2021-22 kwa ushindi mnono wa 6-1

Na MASHIRIKA

HAKIM Ziyech alifunga mabao matatu na kusaidia Chelsea kusajili ushindi wa 6-1 dhidi ya Peteborough kwenye mchuano wa kirafiki wa kujiandaa kwa kampeni za msimu mpya wa 2021-22.

Mchuano huo uliochezewa Julai 17, 2021 katika uwanja wa Cobham ambao hutumiwa na Chelsea kwa mazoezi yao ya kila siku.

Kwa kuwa idadi kubwa ya wanasoka mahiri wangali likizoni baada ya kuwajibishwa na timu zao za taifa kwenye fainali zilizopita za Euro, kocha Thomas Tuchel alihiari kuwapa chipukizi wengi fursa ya kudhihirisha utajiri wa vipaji vyao uwanjani.

Mechi hiyo pia ilitoa fursa kwa viungo Danny Drinkwater na Ross Barkley kuvalia tena jeza za Chelsea baada ya makali yao kushuka pakubwa muhula uliopita.

Tuchel alikumbatia mfumo wa 3-4-3 katika mchuano huo uliomshuhudia akimwajibisha kipa chipukizi Wayne Cumming katikati ya michuma kabla ya nafasi yake kutwaliwa na ucas Bergstrom.

Trevoh Chalobah, Jake Clarke-Salter, Malang Sarr waliwajibishwa nyuma ya Davide Zappacosta na Marcos Alonso waliotegemewa pembezoni.

Mabao mengine ya Chelsea yalifumwa wavuni kupitia Tammy Abraham, Christian Pulisic na Callum Hudson-Odoi.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kikwetu FC yatoka nyuma na kuipiga FC Talents 2-1

Miaka 10 baada ya ugonjwa wa Rinderpest kuondolewa duniani,...