• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 4:40 PM
Kikwetu FC yatoka nyuma na kuipiga FC Talents 2-1

Kikwetu FC yatoka nyuma na kuipiga FC Talents 2-1

Na PATRICK KILAVUKA

KATIKA jukwaa la soka, Kikwetu FC ilitoka nyuma na kuichabanga FC Talents 2-1 katika mchuano mmojawapo wa kuwinda ubabe wa kanda ya Nairobi Magharibi uwanjani Kihumbuini, Jumamosi.

Japo FC Talents ilifunga goli safi kutoka kwa Patrick Kegode dakika ya 20, furaha yao hakudumu pale ambapo Hillary Muhindi alifunika shuti kali na kuyeyesha matumaini ya Talents.

Bao la Alonje Mago ambalo lilididimiza Talents lilipachikwa dakika ya 51.

Katika mchuano mwingine wa Ligi hiyo, Kibagare Slums iliizaba Hillside FC ya Ngong 1-0.

Katika kipindi cha kwanza, timu zote zilikuwa zimekabana koo ya sare tasa kabla Slums kuzua mbinu ya kujizatiti na dakika ya 47 ilizaa matunda baada ya Joseph Kinyanjui kuacha kipa hoi. Hata hivyo, timu zote zilipoteza nafasi nyingi tu za wazi.

Nayo Kipande FC ilikataa kumegeka kwa kutoka sare tasa dhidi ya Lopez FC.

Mchuano wa kaunti ndogo, FKF, Nairobi Magharibi, FC Talents Youth ilipata afueni baada ya kuiliza Kangemi PAG 1-0.

Vincent Bukachi ndiye alipeperusha bendera ya Youth kwa kutia kimiani bao hilo la ushindi dakika ya 33.

PAG ilijitahidi kusawazisha lakini haikufanikiwa.

  • Tags

You can share this post!

Shujaa yafanya mazoezi ya kwanza mbele ya mashabiki Japan

Chelsea waanza kujiandaa kwa msimu mpya wa 2021-22 kwa...