• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Chelsea wakabwa koo na Burnley katika EPL ugani Stamford Bridge

Chelsea wakabwa koo na Burnley katika EPL ugani Stamford Bridge

Na MASHIRIKA

VIONGOZI wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Chelsea, walipoteza alama mbili muhimu katika mechi iliyowashuhudia wakiambulia sare ya 1-1 dhidi ya Burnley ugani Stamford Bridge.

Kai Havertz alifunga bao la Chelsea baada ya kushirikiana na Reece James. Goli hilo lilikuwa la pili kwa Havertz katika kampeni za EPL msimu huu.

Chelsea wangefunga mabao zaidi katika kipindi cha pili ila juhudi za Thiago Silva na Callum Hudson-Odoi zikazimwa na kipa Nick Pope.

Burnley walisawazisha mambo kupitia Matej Vydra aliyekamilisha krosi iliyokuwa zao la ushirikiano mkubwa kati ya Ashley Westwood na Jay Rodriguez.

Kufikia sasa, Chelsea wanaselelea kileleni mwa jedwali la EPL kwa alama 26, tatu zaidi kuliko mabingwa watetezi Manchester City. Kwa upande wao, Burnley wanakamata nafasi ya 18 kwa alama nane na ni miongoni mwa vikosi vitatu vinavyovuta mkia wa jedwali.

Kwa kuambulia sare dhidi ya Burnley, rekodi ya Chelsea ya kushinda mechi nne mfululizo za EPL na saba mfululizo katika mashindano yote ilifikia tamati.

Chini ya kocha Thomas Tuchel, Chelsea wametandaza mechi tatu zilizopita bila kujivunia huduma za wavamizi tegemeo Romelu Lukaku na Timo Werner wanaouguza majeraha.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Real Madrid yakung’uta Rayo Vallecano na kutua...

‘NYS haijatwaa usimamizi wa Kemsa’

T L