• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Chelsea wapoteza alama muhimu katika EPL baada ya kuambulia sare ya 1-1 dhidi ya Nottingham Forest

Chelsea wapoteza alama muhimu katika EPL baada ya kuambulia sare ya 1-1 dhidi ya Nottingham Forest

Na MASHIRIKA

UTEPETEVU wa Chelsea uliruhusu Nottingham Forest kutoka nyuma na kulazimishia mabingwa hao wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) sare ya 1-1 mnamo Jumapili ugani City Ground.

Beki mzoefu Serge Aurier alifunga bao kunako dakika ya 63 na kusaidia Forest kufuta juhudi za Raheem Sterling aliyewaweka Chelsea uongozini katika dakika ya 16.

Ni alama ya kwanza kwa Forest ya kocha Steve Cooper kujizolea baada ya kujipata chini msimu huu. Kikosi hicho sasa hakijapigwa katika mechi sita mfululizo za mashindano yote.

Matokeo hayo yalipaisha Forest hadi nafasi ya 18 jedwalini kwa alama 14 sawa na West Ham United ya kocha David Moyes. Ni pengo la alama moja pekee ndilo linatamalaki kati ya Forest na Wolves wanaokamata nafasi ya 19. Southampton wanavuta mkia wa jedwali kwa pointi 12.

Chelsea ambao wameshinda mechi mbili mfululizo ligini mara moja pekee chini ya kocha Graham Potter aliyeajiriwa Septemba 8, 2022, sasa wanashikilia nafasi ya nane kwa alama 25 sawa na Fulham. Pengo la alama saba linatamalaki kati yao na Manchester United wanaofunga mduara wa nne-bora.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

  • Tags

You can share this post!

Aston Villa washiba sifa za kocha wao Unai Emery baada ya...

SHINA LA UHAI: Wadau kikaoni wahimiza hatua zaidi kupigwa...

T L