• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 7:50 AM
Cristiano Ronaldo afikisha mabao 700 tangu aanze kusakata soka katika ngazi ya klabu

Cristiano Ronaldo afikisha mabao 700 tangu aanze kusakata soka katika ngazi ya klabu

Na MASHIRIKA

CRISTIANO Ronaldo alifunga bao lake la 700 katika ngazi ya klabu na kusaidia waajiri wake Manchester United kutoka nyuma na kukomoa Everton 2-1 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Jumapili.

Nyota huyo raia wa Ureno aliletwa ugani katika kipindi cha kwanza kujaza pengo la Anthony Martial aliyepata jeraha. Bao la Ronaldo lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na Carlos Casemiro.

Ilikuwa mara ya kwanza tangu 2005 kwa Ronaldo, 37, kufunga bao ugani Goodison Park. Man-United alifungiwa bao la kwanza na sajili mpya Antony dos Santos aliyefuta juhudi za Alex Iwobi aliyewaweka Everton kifua mbele mwanzoni mwa kipindi cha kwanza.

Antony aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa Man-United kuwahi kufunga bao katika michuano yake mitatu ya kwanza katika kipute cha EPL.

Ushindi wa Man-United uliwapaisha hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa jedwali la EPL kwa alama 15, moja nyuma ya Chelsea wanaofunga mduara wa nne-bora.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wabajuni wamwomba rais atatue dhuluma dhidi yao

Chuo Kikuu cha Auburn kumfaa nyota Angella Okutoyi...

T L