• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Dimba la betPawa laelekea Kisumu na Nakuru

Dimba la betPawa laelekea Kisumu na Nakuru

NA JOHN ASHIHUNDU

BAADA ya fainali za kanda ya Nairobi kufana Jumapili, ngarambe ya betPawa itaelekea Kisumu wikendi ijayo kwa fainali ya kanda ya Nyanza.

Mechi hizo ziliandaliwa uwanja wa Astro Turf ambapo zaidi ya timu 50 ziliwania taji kwa siku mbili.

Akiba FC iliibuka bingwa baada ya kuliza Pirates FC 2-1.

Walipata kombe na Sh200,000 nayo Pirates ikapokea Sh100,000.

Washindi wa zoni ya Nairobi, Akiba FC, taji na hundi baada ya timu hiyo kupiga Pirates FC 2-1 katika fainali ya kusisimua ya BetPawa Six-Aside iliyosakatwa katika uga wa Jamhuri Astro Turf mnamo Jumapili. PICHA | JOHN ASHIHUNDU

Baada ya Kisumu dimba litatua Nakuru wikendi itakayofuata kwa fainali za Rift Valley.

Mshirikisho wa mauzo wa betPawa Kenya, Simon Mwangi amesema baada ya mashindano ya kufana mwishoni mwa wiki, kampuni hiyo ya Kamari inatarajia mashabiki wengi kuhudhuria fainali ya Kisumu wikendi ijayo.

Bw Mwangi alikuwa akizungmza na mashabiki waliohudhuria fainali ya Kanda ya Nairobi katika viwanja vya Astro Turf, Ngong Road, Jumapili,

Mwangi alisema mpango wa kampuni hiyo ya bahati nasibu unakusudia kuinua vipaji vya vijana kuanzia mashinani kote nchini.

Mwangi alisema mashindano ya mwaka huu yanalenga kugundua vijana katika maeneo ya Nairobi, Kisumu na Nakuru ili baadhi ya vijana hao wapewe ufadhili kwa lengo la kukuza talanta yao.

Kulingana na afisa huyo, betPawa Kenya itatenga kiasi cha kutosha kuanzia mwaka 2024, mbali na vifaa vifaa vya michezo kuwasaidia vijana.

Baada ya fainali za Kisumu zitakazofanyika Jumamosi na Jumapili, mashindano mengine yatafanyika Nakuru kati ya April 15 na 16.

Zaidi ya timu 50 ziliwania ubingwa wa Nairobi ambako Akiba FC iliibuka mabingwa baada ya kuitandika Pirates FC 2-1.

Katika nusu-fainali, Akiba iliibwaga Kuta Collections 3-1 kupitia kwa mikwaju ya penaltii baada ya timu hizo kutofungana katika muda wa kawaida.

Kwa upande mwiungine, Pirates waliibandua Lamasia 5-4 pia kupitia kwa matuta baada ya timu hizo kuagana kwa 0-0 katika muda wa kawaida.

Mabao ya Akiba yalifungwa na Mohamed Hassan na Bol Peter wakati Eugen Wethuli akifungia Pirates kabla ya kutawazwa mchezaji bora wa mashindano hayo.

Mbali na Kombe, Akiba walipokea Sh200,000, Pirates wakapata Sh100,000 wakati Kuta Collections wakiondoka na Sh50,000 baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu kutokana na ushindi wao wa 2-1 dhidi ya Lamasia. Timu zote nne zilipokea mavazi rasmi ya kimichezo baada ya kutinga nusu-fainali.

BetPawa pia huendesha shughuli zake katika mataifa ya Nigeria, Uganda, Ghana, Tanzania, Cameroon DRC Congo, Malawi na Ruanda.

  • Tags

You can share this post!

Leicester City mawindoni kusaka kocha mpya

Erick Omondi ashtakiwa kwa usumbufu na kupiga nduru jijini

T L