• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
UDAKU: Essien na mkewe Akosua Puni wamerejesha tena mahaba

UDAKU: Essien na mkewe Akosua Puni wamerejesha tena mahaba

IMEKUSANYWA NA CHRIS ADUNGO

MWANASOKA wa zamani wa Chelsea na timu ya taifa ya Ghana, Michael Essien, 39, hatimaye amerudiana na mkewe Akosua Puni ambaye ni mzawa wa Ghana na raia wa Uingereza.

Wawili hao walitengana 2019 baada ya mwigizaji wa Gambia, Princess Shyngle, 31, kufichua alivyokuwa akila uroda na Essien kisiri.

Awali, Akosua, ambaye ni mama wa watoto wawili – Michelle na Michael Jr – alikuwa amekataa kabisa kufanya gumzo na ujumbe maalumu uliokuwa ukitumwa na Essien mara kwa mara kuwapatanisha.

Essien ambaye pia amewahi kuvalia jezi za Bastia, Olympique Lyon, Real Madrid na AC Milan, sasa ni kocha msaidizi wa kikosi cha FC Nordsjaelland nchini Denmark na mkewe ni mmiliki wa kikosi cha FC Cosmo nchini Italia.

Kabla ya kuanza kumtambalia Princess kisiri, Essien aliwahi pia kuchepuka na mwigizaji mashuhuri mzawa wa Ghana, Nadia Buari ambaye kwa sasa ni mama wa watoto wawili wa kike.

“Kosa la Essien halikuwa la kusameheka. Niliwazia suala la kurudiana naye kwa kipindi kirefu na nikahisi moyo ukiwa mzito. Sikutaka kupenda tena lakini mtu hapigani vita na nguvu za mapenzi akashinda,” akasema Akosua.

Princess aliyetemana rasmi na mumewe Gibou Bala Gaye mnamo Aprili 2021, sasa anamnyemelea kimapenzi mwanasoka wa zamani wa AS Monaco, Arsenal, Man-City, Real Madrid, Tottenham na Crystal Palace, Emmanuel Adebayor. Sogora huyo raia wa Togo sasa ni kapera baada ya kuachana na kipusa raia wa Namibia, Dillish Mathews, mnamo Novemba 2019.

You can share this post!

Kikosi kipya kuweka ulinzi uchaguzini

Hali ngumu kuandama Wakenya 2022

T L