Na MASHIRIKA
ERLING Haaland alifunga mabao mawili na kusaidia Manchester City kufungua kampeni zao za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu kwa ushindi mnono wa 4-0 dhidi ya Sevilla ya Uhispania mnamo Jumanne usiku.
Haaland aliwafungulia Man-City ukurasa wa mabao katika dakika ya 20 baada ya kushirikiana vilivyo na kiungo Kevin de Bruyne. Goli hilo lilikuwa lake la 11 kutokana na mechi nane tangu asajiliwe na Man-City kutoka Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Aliongeza bao la pili la mechi katika dakika ya 67 baada ya Phil Foden kufungia Man-City goli la tatu kunako dakika ya 58. Bao la nne la masogora wa kocha Pep Guardiola lilijazwa kimiani na beki Ruben Dias aliyemzidi ujanja kipa Yassine Bounou.
Ushindi huo wa Man-City uliwakweza kileleni mwa Kundi G. Dortmund waliokung’uta FC Copenhagen ya Denmark 3-0 wanakamata nafasi ya pili.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO