• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Jackson Mutiso ashinda Sh20 milioni za SportPesa Midweek Jackpot

Jackson Mutiso ashinda Sh20 milioni za SportPesa Midweek Jackpot

Na CECIL ODONGO

ILIKUWA furaha riboribo kwa Jackson Mutiso kutoka Athi River, Kaunti ya Machakos baada ya kushinda Sh20 milioni kwenye SportPesa Midweek Jackpot.

Mutiso, ambaye ni yatima na ana familia ya watoto watatu, alishindwa kuzungumza vyema na nusura adondokwe na machozi alipokabidhiwa hundi yake katika hafla ya kipekee iliyoandaliwa na SportPesa katika mkahawa wa Stanley Sarova, Nairobi.

Mutiso alitabiri vyema mechi zote 13 kati ya 13 na kufanikiwa kushinda pesa hizo ambazo zilimwezesha kuwa milionea mpya. Mwenzake David Murimi ambaye alishinda Sh2.1 milioni kwenye Mega Jackpot, pia alituzwa wakati wa hafla hiyo ya kusisimua.

“Sina mengi ya kuyasema kwa sababu nimefurahi sana. Vile mnaniona hapa, mimi ni mwekezaji mkubwa wa SportPesa. Nimekuwa nikicheza kamari ya SportPesa kwa muda wa miaka minne iliyopita. Taarifa hizi zilinipata nikiwa kwenye nyumba ninakoishi pekee yangu kwa kuwa mke wangu na watoto wangu wako mashinani,” akasema Bw Mutiso.

“Nalenga kutumia pesa hizo kununua ploti kisha kujenga nyumba. Nitaendelea kucheza kwa sababu nalenga mamilioni zaidi,” akaongeza.

Murimi naye alifurahi akisema kuwa amekuwa akicheza kwa muda wa miaka saba iliyopita ila amekuwa akishinda pesa kidogo kabla ya dua ya Sh2.1 milioni kumwaangukia. Alitabiri mechi 15 kati ya 17 na kushinda pesa hizo.

Meneja wa shughuli za SportPesa Bernard Chauro aliwapongeza wawili hao akisema kuwa kampuni hiyo itaendelea kuwafurahisha wateja wake kwa haki na ukweli.

“Tutatembea na wewe Mutiso. Leo tumekuja hadi mahali unafanya kazi na tutahakikisha kuwa tunakufuatilia ili utumie pesa hizi vizuri,” akasema.

  • Tags

You can share this post!

Ashtakiwa kwa madai ya kusaidia mtoto kuavya mimba

Bandari za Mombasa na Lamu zapata kreni za kielektroniki

T L