• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Jepkorir, Mateiko kuwa kivutio mbio za nyika za Discovery Kenya wikendi

Jepkorir, Mateiko kuwa kivutio mbio za nyika za Discovery Kenya wikendi

BERNARD ROTICH na GEOFFREY ANENE

NYOTA Brilliant Jepkorir amethibitisha kutimka katika makala ya 31 ya mbio za nyika za Discovery Kenya katika klabu ya michezo ya Eldoret, Uasin Gishu hapo Jumapili.

Bingwa huyo wa 2019 atapimwa vilivyo weledi wake dhidi ya bingwa mtetezi Daisy Cherotich.

Pia atakuwepo mshindi Beirut Marathon 2017 Eunice Chumba kutoka Bahrain aliyekamata nafasi ya tatu mwaka jana, mshindi wa Frankfurt Marathon 2019 Valary Aiyabei, malkia wa Valencia Marathon 2021 Nancy Jelagat na bingwa wa dunia mbio za nyika 2017 Irene Cheptai.

Jepkorir alieleza Taifa Spoti kuwa amepumzika vyema baada ya mbio za nyika za kitaifa Januari 22. Amezamia mazoezi mjini Iten, Elgeyo Marakwet.

“Nilikamata nafasi ya 11 wikendi iliyopita. Zilikuwa mbio ngumu.

“Sasa niko sawa na nitajaribu kukamilisha mbio za nyika za Discovery Kenya katika nafasi tatu za kwanza, ingawa najua ushindani utakuwa mkali,” alisema Jepkorir.

Kitengo cha wanaume kimevutia Daniel Mateiko, Titus Kiprotich na Emmanuel Bor.

Robert Kiprop alinyakua taji 2021 akifuatiwa na mshindi 2o20 Nicholas Kimeli, na mshindi wa medali ya michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka 2018 Rodgers Kwemoi.

  • Tags

You can share this post!

Kibarua sugu chasubiri Shujaa ikielekea mawindoni Seville 7s

Raila, mashabiki walaani mauaji ya kipenzi Juma

T L