• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 6:50 AM
Jinsi wachezaji wa kigeni walivyong’aa mashindano ya chesi 2023

Jinsi wachezaji wa kigeni walivyong’aa mashindano ya chesi 2023

NA AREGE RUTH

GRANDMASTER (GM) Timur Gareyev wa Amerika na Mjerumani Mwanamke Grandmaster (WGM) Josefine Heinemann ndio mabingwa wa mashindano ya Sataranji ya Kenya Open ya mwaka 2023.

Mashindano hayo yaliokamilika Jumatatu, Aprili 10, 2023 katika ukumbi wa Sarit Expo jijini Nairobi yalivutia washiriki 374 kutoka mataifa 22 kote duniani.

Gareyev, ambaye alijinyakulia alama (2602) alitia mfukoni Sh1 milioni kwa ushindi wake katika kitengo cha Open huku Heinemann (2274) akipokea Sh500,000 kwa kung’aa upande wa wanawake.

“Kusema kweli, nilipata bahati kubwa katika mashindano haya. Wapinzani wangu wote walikuwa wakali sana,” alisema Timur.

Timur 35 ni gwiji katika chesi. Ameshinda mataji mengi ya kimataifa yakiwemo mashindano ya America Open mwaka 2016 na mashindano ya 2018 ya chesi ambayo yaliandaliwa Marekani Kaskazini.

Katika nafasi ya 17 na pointi saba, Mkenya mwalimu na nahodha wa Kenya Ben Magana ndiye alikuwa mchezaji bora.

Katika kitengo cha wanawake, kilichokuwa na washiriki 92, Heinemann alishinda raundi zote tisa. Alifuatwa na Misri Wafa Shrook (2138), na Wafa Shaheda (2099) wote waliofungana kwa pointi 7.5 pamoja na Mganda Gloria Nansubuga (1459).

Katika nafasi ya tano na pointi saba kitengo cha wanawake, Wakenya Sasha Mongeli (1695) na Joyce Nyaruai ambaye alijinyakulia alama (1662) walikuwa wachezaji bora wa Kenya.

  • Tags

You can share this post!

Ndindi Nyoro aahidi bajeti ya 2023/24 itaweka zingatio kwa...

JURGEN NAMBEKA: Heko Mwadime kutimua wafisadi ila uozo...

T L