• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Johana Omondi aanza maisha Ubelgiji kwa ushindi

Johana Omondi aanza maisha Ubelgiji kwa ushindi

Na GEOFFREY ANENE

KIUNGO mshambulizi Eric Johana Omondi alianza maisha Waasland-Beveren kwa ushindi baada ya klabu hiyo yake mpya kulima Virton 3-1 Jumapili usiku.

Herve Kage aliweka Virton kifua mbele dakika ya 20 kabla ya wenyeji Waasland-Beveren kujibu na magoli matatu katika kipindi cha pili kupitia kwa Daniel Maderner (mawili ikiwemo penalti) na Kevin Hoggas. Omondi alijaza nafasi ya Abdel Al Badaoui dakika ya 87. Alilishwa kadi ya njano katika dakika saba alipata kucheza.

Omondi alijiunga na Waasland-Beveren inayoshiriki ligi ya daraja ya pili Ubelgiji kutoka Jonkoping Sodra ya uswidi mnamo Januari 26 kwa kandarasi ya miezi sita.

Waasland-Beveren ni klabu ya nne ya kigeni kwa Omondi baada ya kuwasili huko kwa mara ya kwanza mwaka 2017 kuchezea Vasalund nchini Uswidi.

Mwaka 2018, alijiunga na Brommapojkarna kabla ya kuelekea Jonkoping mwaka 2020 alikofanya vyema. Alitinga mabao 14 na kusuka pasi tatu zilizozaa matunda katika michuano 55 kambini mwa Jonkoping kabla ya kuelekea Waasland-Beveren.

Klabu yake mpya inashikilia nafasi ya tatu kwa alama 36 kutokana na michuano 23 nayo Virton inakamata mkia kwa alama 14.

  • Tags

You can share this post!

Mung’aro aanza kumponda Kingi

Klopp ataka Liverpool kujihadhari dhidi ya Inter Milan...

T L