• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:50 AM
Kaizer Chiefs yapepetwa 4-0 na Wydad Athletic

Kaizer Chiefs yapepetwa 4-0 na Wydad Athletic

Na GEOFFREY ANENE

Mkenya Anthony ‘Teddy’ Akumu alisakata mechi nzima timu yake ya Kaizer Chiefs ikiaibishwa 4-0 mikononi mwa wenyeji Wydad Athletic kwenye Klabu Bingwa Afrika, Jumapili.

Katika mechi hiyo ya Kundi C iliyochezewa uwanjani Agosti 4 nchini Burkina Faso, Chiefs ilizamishwa na magoli kutoka kwa Mohamed Ounajem dakika ya saba, Ayoub El Kaabi (44), Mtanzania Simon Msuva (86) na Yahya Jabrane (90+2).

Jabrane alifunga penalti iliyopatikana baada ya beki Ramahlwe Mphahlele kulishwa kadi yake ya pili ya njano katika mchuano huo aliponawa mpira. Wydad kutoka Morocco imekalia juu ya jedwali kwa alama sita.

Ilipepeta Petro de Luanda (Angola) 1-0 viungani mwa jiji la Luanda mnamo Februari 23. Horoya ni ya pili kwa alama nne baada ya kuchabanga Petro de Luanda 2-0 mnamo Februari 13 jijini Conakry.

Chiefs ina alama moja nayo Petro de Luanda haina kitu. Timu ya Chiefs itaalika Petro de Luanda mnamo Machi 6, siku ambayo Wydad pia itakuwa mwenyeji wa Horoya.

  • Tags

You can share this post!

Tisho la baa la njaa kutokana na ukosefu wa maji Lamu

Tumepiga hatua ya maana, asema kocha wa Shujaa