• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Kakamega kumkosa kuingo Francis Omondi

Kakamega kumkosa kuingo Francis Omondi

Na JOHN KIMWERE

HUENDA Kakamega Homeboyz itakosa huduma za kiungo, Francis Omondi kwenye mechi zilizosalia za Ligi Kuu ya Soka la Kenya (FKF-PL) muhula huu.

Kiungo huyo alifanyiwa upasaji mwezi Novemba mwaka uliyopita ambapo hadi sasa hajarejea kushiriki mazoezi na wachezaji wenzake. ”Sina shaka kutaja kuwa kiungo huyo ni kama hatarejea kushiriki mechi za msimu huu ambapo hatuna budi kumruhusu pia kumpa muda tosha wa kupumzika na apone,” kocha Bernard Mwalala alisema na kuongeza kuwa itabidi wenzake wajikaze kufunika mwanya huo maana alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi chake.

Tayari Kakamega imetwaa huduma za Evans Maliachi akitokea FC Talanta ya kocha Ken Kenyatta. Mchezaji huyo amewahi kuchezea Sofapaka FC, Nzoia Sugar na Nakuru All Stars. Kando na Evans Maliachi Kakamega inayoongoza katika jedwali la Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF-PL) imesajili Mike Isabwa kutoka Vihiga Bullets na Gaetan Masha akitokea Nzoia Sugar.

Kwenye ratiba ya kipute hicho Kakamega Homeboyz inayozidi kufanya kweli kesho itaingia mzigoni kucheza na Nzoia Sugar FC. Katika msimamo wa kinyang’anyiro hicho, Kakamega ingali kifua mbele kwa kuzoa alama 33, nne mbele ya KCB. Kariobangi inafunga tatu bora kwa kusajili pointi 28 sawa na City Stars maarufu Nairobi Simba tofauti ikiwa idadi ya mabao huku Gor Mahia ikifunga tano bora kwa alama 27.

You can share this post!

Covid-19: Utafiti waonyesha kafyu na ‘lockdown’...

TUSIJE TUKASAHAU: Uhuru asije akasahau serikali yake...

T L