• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 10:55 AM
Kocha wa Harambee Starlets ana kibarua kuteua timu ya mwisho

Kocha wa Harambee Starlets ana kibarua kuteua timu ya mwisho

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa timu ya wanawake ya Harambee Starlets, Alex Alumirah ana mtihani mzito kuteua kikosi cha mwisho kitakaocheza na Uganda kwenye mechi mbili za kufuzu kushiriki fainali za Kombe la Afrika (AWCON).

Licha ya utata unaozingira mechi hizo, Starlets imepangwa kusafiri nchini Uganda kucheza na wenyeji wao Crested Cranes Februari 16 kisha kuwaalika majirani hao hapa nchini wiki moja baadaye.

Alumirah ambaye hufunza Tiger Queens nchini Tanzania anasaidiana na Berta Achieng (Thika Queens) na Ann Aluoch (Mathare Women FC).

”Bila shaka tunakabiliwa na kibarua kigumu lakini tunatarajia kuteua kikosi imara na tayari kufanya kweli,” alisema na kuongeza kuwa mchezaji yoyote yupo kambini anayo nafasi ya kuteuliwa katika kikosi cha mwisho ubora wao ndio utakaotegemea.

Makocha hao wana mtihani hasa kwa wachezaji wa safu ya mbele. Orodha ya walioitwa kambini inajumuisha Tereza Engesha mchezaji wa Vihiga Queens aliyeibuka mfungaji bora msimu wa 2019 alipocheka na wavu mara 36.

Pia mchana nyavu huyo kwa mara nyingine yupo fiti ambapo kwenye kampeni za msimu huu amefungia klabu yake mabao tisa baada ya kushiriki mechi saba.

Pia yupo mvamizi na winga Mwanahalima Adam ambaye akipigia Thika Queens msimu uliyopita aliibuka mfungaji bora kwa kutikisa nyavu mara 23. Mchezaji huyo kwa sasa anachezea Hakkaragicu ya daraja la Kwanza nchini Uturuki.

Mwingine akiwa Jentrix Shikangwa aliyesafiri nchini Uturuki wiki iliyopita.

Mwanasoka huyo aliibuka mfungaji bora kwenye mechi za CECAFA muhula uliyopita ambapo kabla ya kuondoka majuzi alikuwa amefungia Vihiga Queens mabao sita.

Pia wapo Essie Akida aliyeitwa baada ya kufana anakochezea klabu ya PAOK nchini Ugiriki.

Kadhalika wapo wanasoka wawili wa Gaspo Women Mercy Airo na Elizabeth Wambui wanaokuja kivingine kwa kutikisa nyavu.

Wawili hao ni kati ya wachezaji wanaofungia timu hiyo mabao kwenye kampeni za msimu huu ambapo wamesaidia kutua katika nafasi ya pili kwenye jedwali.

You can share this post!

JIJUE DADA: Chanzo cha vidutu kwenye tupu ya nyuma

Wakongwe walalamikia foleni ndefu wakati wa malipo ya Inua...

T L