• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
KWPL: Wadadia FC yaponea kuangukiwa na shoka

KWPL: Wadadia FC yaponea kuangukiwa na shoka

NA JOHN KIMWERE

WADADIA FC imeponea kushushwa ngazi kutoka Ligi Kuu ya Soka la Wanawake (KWPL) baada ya kulazimisha sare tasa dhidi ya mabingwa wa kipute hicho, Vihiga Queens ugani Mumias Complex.

Wadadia chini ya kocha, Rashid Sumba ilishusha mechi safi dhidi ya wapinzani wao kinyume na ilivyokuwa kwenye mechi za mkumbo wa kwanza ilipolazwa mabao 8-1. Nayo Ulinzi Starlets ilitoka nguvu sawa bao 1-1 na Gaspo Womens.

Thika Queens ilidungwa bao 1-0 na Kisumu Allstars huku Bunyore Starlets ikizoa mabao 4-2 mbele ya Kangemi Starlets.

Gaspo Women ilitangulia kupata bao hilo kupitia Bertha Omita kabla ya Mercy Airo kusawazishia Maafande wa Ulinzi Starlets. Licha ya Vihiga kutoka sare inaedeleza rekodi ya kutoshindwa kwenye mechi za kipute hicho muhula huu.

Vihiga ya kocha, Boniface Nyamunyamu iliyotwaa taji hilo wiki tatu zilizopita ilipata nafasi ya kwanza kunako dakika ya tano kupitia nahodha wake, Enez Mango lakini alishindwa kutumia vizuri.

Dakika tano baadaye kupitia Alice Mideri lakini pasi yake iligonga Esther Amakobe. Timu zote ziliwinda angalau bao moja lakini hakuna iliyobahatika.

”Ilikuwa mechi nzuri wapinzani wetu walikaa ng’ang’ari katika safu ya ulinzi na kuzima juhudi za wachezaji wangu,” Nyamunyamu alisema.

”Kusema ukweli kutoka nguvu sawa na Vihiga ni kama ushindi kwangu,” Rashid Sumba alisema na kushukuru wachezaji wake kwa kushusha mechi nzuri dhidi ya mabingwa hao.

Vihiga ingali kifua mbele kwa alama 57, nayo Wadadia inashikilia nafasi ya nane kwa kusajili pointi 23.

  • Tags

You can share this post!

Vihiga Bullets yashushwa ngazi

SHINA LA UHAI: Mzigo wa kansa kwa wazee nchini

T L