• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Vihiga Bullets yashushwa ngazi

Vihiga Bullets yashushwa ngazi

NA JOHN KIMWERE

VIHIGA Bullets imeshushwa ngazi kutoka Ligi Kuu ya FKF-PL baada ya kung’atwa kwa mabao 4-1 na Maafande wa Kenya Police kwenye patashika iliyopigiwa Bukhungu Stadium, Kakamega.

Vihiga Bullets ya kocha, Juma Abdallah iliingia mzigoni kuwinda alama tatu ambazo zingeisaidia kupunguza pengo kati yake na Wazito FC lakini tumaini la wachezaji hao liligonga ukuta.

Police FC ambayo hutiwa makali na kocha, Smmy Omolo ilionyesha soka safi na kupata bao la kwanza dakika ya 28 kupitia juhudi zake Clinton Kinanga.

Dakika nane baadaye David Simiyu alitia kimiani bao la pili baada ya Alvin Mang’eni kuchanja pasi safi. Bullets ilitunukiwa penalti iliyochanjwa na Robert Arrot na kupatia Bullet bao lililosalia la kufuta machozi. Kipindi cha pili, Bullets ilipigana kwa udi na uvumba ikiwinda bao la kusawazisha lakini bahati haikusimama.

Kipindi cha pili, Clifton Miheso alicheka na wavu mara mbili na kutwaa uongozi wa mfungaji bora kwa kufikisha mabao 15. Mchana nyavu huyo alifungia Police bao la tatu dakika ya 75 baada ya kupata pasi yake Duke Abuya kabla ya kumaliza shughuli dakika ya 89.

  • Tags

You can share this post!

Ronaldo asaidia Ureno kuzamisha Uswisi katika pambano la...

KWPL: Wadadia FC yaponea kuangukiwa na shoka

T L