Na MASHIRIKA
MANCHESTER United wamejiondoa katika mbio za kuwania maarifa ya mvamizi Marko Arnautovic kutoka kambini mwa Bologna.
Kocha mpya wa Man-United, Erik ten Hag, amekuwa akifukuzia huduma za Arnautovic – nyota mzoefu raia wa Austria aliyewahi kunolewa na mkufunzi huyo raia wa Uholanzi kambini mwa FC Twente.
Hata hivyo, Man-United wametamatisha azma ya kumsajili Arnautovic baada ya Bologna kudai kiasi kikubwa fedha kwa ajili ya fowadi huyo.
Man-United walifichua mpango wa kumsajili Arnautovic baada ya Brighton kuwapepeta 2-1 katika mchuano wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu wa 2022-23 mnamo Agosti 7, 2022 ugani Old Trafford.
Arnautovic aliwahi kufunga mabao 43 kutokana na mechi 184 akichezea West Ham United na Stoke City kati ya 2013 na 2019.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO