• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Man-United wapepeta Leicester City katika EPL ugani King Power

Man-United wapepeta Leicester City katika EPL ugani King Power

Na MASHIRIKA

MANCHESTER United walisajili ushindi wao wa tatu mfululizo katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) chini ya kocha mpya Erik ten Hag baada ya kutandika Leicester City 1-0 mnamo Alhamisi usiku ugani King Power.

Bao la pekee na la ushindi kwa upande wa Man-United lilijazwa kimiani kupitia kwa Jadon Sancho aliyeshirikiana vilivyo na Marcus Rashford katika dakika ya 23.

Man-United ambao ni mabingwa mara 20 wa EPL walishuka dimbani wakijivunia motisha ya kupepeta Liverpool 2-1 kabla ya kukomoa Southampton 1-0.

Man-United walianza mechi kwa matao ya juu na wakamiliki asilimia kubwa ya mpira katika vipindi vyote viwili vya mchezo. Matokeo hayo yalisaza Leicester ya kocha Brendan Rodgers ambayo haijashinda mechi yoyote ligini msimu huu kwenye mkia wa jedwali la EPL.

Ni mara ya kwanza tangu Aprili 2021 kwa Man-United kushinda mechi tatu mfululizo katika mashindano yote. Kufikia sasa, masogora hao wa Ten Hag wanakamata nafasi ya tano kwenye jedwali la EPL kwa alama tisa, sita nyuma ya Arsenal wanaoselelea kileleni.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

  • Tags

You can share this post!

Kamket atangaza kushirikiana na Kenya Kwanza

Wakenya washauriwa wakome kutumia mitandao ya kijamii...

T L