• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Man-United waripoti visa vingi zaidi vya corona

Man-United waripoti visa vingi zaidi vya corona

Na MASHIRIKA

MANCHESTER United wameripoti visa zaidi vya maambukizi ya Covid-19 baada ya kikosi chao kurejea kambini mwa mazoezi.

United walifunga kambi ya mazoezi ya kikosi chao cha kwanza mnamo Disemba 13, 2021 baada ya ongezeko la visa vya maambukizi ya corona lililoweka mchuano wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kati yao na Brentford uwanjani Old Trafford kuahirishwa.

Mabingwa hao mara 20 wa EPL walirejea kambini mnamo Disemba 15 kwa mazoezi ila bila wachezaji waliokuwa wamefanyiwa vipimo vya afya na kupatikana na virusi vya corona.

Mechi ya EPL iliyokuwa iwakutanishe na Brighton ugani Old Trafford mnamo Disemba 18 tayari imeahirishwa.

Mchuano wa EPL uliokuwa ukutanishe Burnley na Watford ugani Turf Moor mnamo Jumatano uliahirishwa kwa sababu ya corona.

Mchuano huo ulikuwa wa tatu kuahirishwa ligini chini ya kipindi cha wiki moja baada ya nyinginezo kati ya Tottenham Hotspur na Brighton na Brentford na Man-United pia kufutiliwa mbali.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Serikali kutathmini VAT inayotozwa mbegu za mboga

Gretsa yatenga Sh100 milioni za upanuzi wa chuo

T L