• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Masika avuna taji la League Cup nchini Thailand

Masika avuna taji la League Cup nchini Thailand

Na GEOFFREY ANENE

WINGA Ayub Timbe Masika alinyakua taji lake la tatu la msimu 2021-2022 baada ya klabu yake ya Buriram United kulima Prachuap 4-0 katika fainali ya Thai League Cup uwanjani Leo mjini Thanyaburi, Jumapili.

Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Kenya alichezeshwa dakika 78 katika mechi hiyo ambayo waajiri wake walidhibiti kila idara.

Buriram ilichana nyavu za wapinzani wao kupitia kwa raia wa DR Congo Jonathan Bolingi dakika ya 35 na 61, Peeradon Chamratsamee dakika ya 90 na Suphanat Mueanta aliyejaza nafasi ya Masika, dakika ya kwanza ya majeruhi. Prachuap ilikamilisha mechi wachezaji 10 baada ya beki Saharat Pongsuwan kulishwa kadi nyekundu dakika ya 69.

Masika alinyakua taji lake la kwanza wakati Buriram ilinyuka Nongbua Pitchaya 3-0 Aprili 10 ikishinda Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu 2018.

Kisha, mchezaji huyo, ambaye amesakata soka ya malipo Ubelgiji, Uchina, Uingereza na Japan, akapata taji la pili wakati Buriram ililemea Nakhon Ratchasima 1-0 katika fainali ya Kombe la FA uwanjani Thammasat mjini Khlong Luang mnamo Mei 22.

  • Tags

You can share this post!

Gavana wa CBK ahimiza wadau waungane kupiga jeki sekta ya...

Lewandowski asema haoni uwezekano wa kuendelea kuwa...

T L