• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 1:46 PM
Lewandowski asema haoni uwezekano wa kuendelea kuwa mchezaji wa Bayern Munich

Lewandowski asema haoni uwezekano wa kuendelea kuwa mchezaji wa Bayern Munich

Na MASHIRIKA

FOWADI Robert Lewandowski amesema “uhusiano wake na Bayern Munich umefikia kikomo na kubwa zaidi katika mipango yake kwa sasa ni kutafuta hifadhi mpya kwingineko”.

Nyota huyo raia wa Poland angali na mwaka mmoja zaidi kwenye mkataba wake wa sasa na Bayern ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga).

Mwanzoni mwa Mei 2022, Mkurugenzi wa Soka kambini mwa Bayern, Hasan Salihamidzic, alisema kwamba Lewandowski, 33, alikuwa amemfichulia mpango wa kuondoka ugani Allianz Arena.

Lewandowski anahusishwa na uwezekano mkubwa wa kuyoyomea Uhispania kuvalia jezi za Barcelona.

“Kitu kimoja kilicho dhahiri hii leo ni kwamba uhusiano wangu na Bayern umekatika rasmi,” akatanguliza.

“Baada ya vitu vyote ambavyo vimefanyika katika miezi ya hivi karibuni, sioni uwezekano wowote wa kuendelea kuwa mchezaji wa Bayern. Nahisi kwamba kuhamia kwingine kutanipa changamoto mpya itakayoniwezesha hata kuwajibikia timu ya taifa ya Poland ipasavyo,” akaongeza Lewandowski.

Lewandowski aliyehamia Bayern kutoka Borussia Dortmund mnamo 2014, ameshinda mataji manane ya Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) na aliongoza Bayern kunyanyua ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo 2020.

Alifungia Bayern mabao 50 kutokana na mechi 46 msimu huu na anajivunia jumla ya magoli 344 kutokana na michuano 375 katika kipindi cha miaka minane kambini mwa Bayern. Ndiye wa pili nyuma ya marehemu Gerd Muller katika orodha ya wafungaji bora wa muda wote kambini mwa Bayern.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Masika avuna taji la League Cup nchini Thailand

Beki Marcelo kuondoka Bernabeu akiwa mchezaji anayejivunia...

T L