• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Masika na timu yake ya Vissel Kobe waaga Levain Cup

Masika na timu yake ya Vissel Kobe waaga Levain Cup

Na GEOFFREY ANENE

VISSEL Kobe anayochezea Ayub Masika imebanduliwa kwenye kipute cha Levain Cup kwa jumla ya mabao 4-3 baada ya kutoka 2-2 katika mechi ya marudiano ya robo-fainali dhidi ya Urawa Red Diamonds, Jumapili.

Wenyeji Urawa walitangulia kuona lango dakika ya 16 kupitia kwa Yoshio Koizumi. Mbrazil Douglas alisawazisha 1-1 dakika sita baadaye kabla ya Urawa kuenda mapumzikoni kifua mbele 2-1 baada ya Kasper Junker kuongeza la pili dakika ya 45.

Winga Mkenya Masika aliingia katika nafasi ya Ryo Hatsuse dakika ya 71. Dakika sita baadaye, kiungo stadi kutoka Uhispania, Andres Iniesta alisawazisha 2-2. Juhudi za Vissel kupata bao la tatu mbele ya mashabiki 4,892 ziligonga mwamba.

Vissel ya kocha Atsuhiro Miura ilipoteza mechi ya mkondo wa kwanza 2-1 katika uwanja wake wa nyumbani wa Noevir mjini Kobe mnamo Juni 6.

Timu ya Vissel sasa inaelekeza juhudi zake kwa kipute cha Emperor’s Cup dhidi ya Suzuka Unlimited mnamo Juni 16.

  • Tags

You can share this post!

Ondoa gharama ya kununua fatalaiza kwa kujitengezea mbolea...

Uingereza wakomoa Croatia katika mechi ya kundi D kwenye...