• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
McGrath ataja 15 kwa duru ya kufa-kupona ya Toulouse 7s

McGrath ataja 15 kwa duru ya kufa-kupona ya Toulouse 7s

Na GEOFFREY ANENE

KOCHA Damian McGrath amekimbilia huduma za Denis Abukuse na Ronald Omondi kuokoa Kenya Shujaa kutoka minyororo ya kuaga Raga za Dunia.

Mwingereza huyo mnamo Ijumaa amejumuisha Abukuse katika kikosi cha wachezaji 15 kwa duru ya Ufaransa na Uingereza baada ya kukosa Hong Kong na Singapore mwezi uliopita. Katika msimu wake wa kwanza, Abukuse ana miguso sana na amechangia jumla ya pointi 43 katika mechi 30.

Ronald amekosa duru nne zilizopita.

Shujaa inakamata nafasi ya 13 kwa alama 37, 11 ndani ya mduara hatari.

Inahitaji kufika nusu-fainali mjini Toulouse Mei 12-14 na kuomba Uruguay na Uhispania wafanye vibaya ili ijikwamue.

Shujaa itapepetana na Uruguay na New Zealand mnamo Mei 12 na Canada (Mei 13) katika Kundi A. Nahodha wa zamani Humphrey Kayange alisema Shujaa itajitahidi kutafuta matokeo mazuri isibanduliwe.

Kikosi cha Kenya Shujaa:

Nelson Oyoo (nahodha), Herman Humwa, Edmund Anya, Brian Tanga, Johnstone Olindi, Alvin Otieno, Kevin Wekesa, Jeffrey Oluoch, John Okoth, George Ooro, Daniel Taabu, Denis Abukuse, Billy Odhiambo, Ronald Omondi, Anthony Omondi.

  • Tags

You can share this post!

Rais Ruto amwomboleza Mukami Kimathi

‘Mhubiri’ Paul Mackenzie kuendelea kuzuiliwa...

T L