• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Mechi ya UEFA kati ya Real Madrid na Liverpool kuchezewa Uhispania baada ya kanuni za Covid-19 kulegezwa

Mechi ya UEFA kati ya Real Madrid na Liverpool kuchezewa Uhispania baada ya kanuni za Covid-19 kulegezwa

Na MASHIRIKA

MCHUANO wa mkondo wa kwanza wa robo-fainali kati ya Real Madrid na Liverpool hautahamishiwa kwingineko baada ya Uhispania kulegeza masharti ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.

Mnamo Disemba, Uhispania ilisitisha safari kutoka Uingereza kutokana na ongezeko la visa vya maambukizi mapya ya corona. Jambo hilo liliwaweka vinara wa Shirikisho la soka ya bara Ulaya (Uefa) katika ulazima wa kuhamishia kwingineko mechi za UEFA na Europa League zilizohusisha Chelsea na Manchester United.

Masharti makali ya kudhibiti virusi vya corona yaliyowekwa na Uhispania yanatarajiwa kukamilika mnamo Machi 30 huku Real wakitazamiwa kupepetana na Liverpool uwanjani Alfredo di Stefano katika raundi ya kwanza mnamo Aprili 6.

Mechi ya robo-fainali ya Europa League kati ya Granada na Man-United pia itachezewa Uhispania mnamo Aprili 8, 2021.

Mbali na Uhispania, Ujerumani pia iliweka vikwazo kuhusu usafiri kutoka Uingereza, jambo lililochangia mechi za hatua ya 16-bora za UEFA kati ya Manchester City na Borussia Monchengladbach, kisha Liverpool na RB Leipzig zikihamishiwa jijini Budapest, Hungary.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

CHAWAKAMA KENYA: Kiswahili kwa maendeleo endelevu

AK yaahirisha mbio za kupokezana vijiti za kuchagua timu ya...