NA MASHIRIKA
MKE wa nyota wa PSG Achraf Hakimi, Hiba Abouk amewasilisha kesi ya talaka, akidai zaidi ya nusu ya mali na utajiri wa mumewe.
Alipofika mahakamani, iligundulika kwamba Achraf Hakimi alikuwa amesajili mali yake yote chini ya jina la mama yake mzazi.
Asilimia 80 ya Euro Milioni 1 anazopokea kutoka PSG kila mwezi huwekwa kwenye akaunti ya mamake.
Cha kushangaza ni kuwa, mchezaji wa timu ya taifa ya Morocco mali yake yote yakiwemo, magari, nyumba, vito vya thamani vyote vimeandikishwa kawa jina la mamake na si lake.
TAFSIRI NA AREGE RUTH