• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Mwamba RFC ni wafalme wa Driftwood 7s

Mwamba RFC ni wafalme wa Driftwood 7s

Na GEOFFREY ANENE

KLABU ya Mwamba imetwaa ubingwa wa duru ya tatu ya raga ya kitaifa ya wachezaji saba kila upande ya Driftwood jijini Mombasa, Jumapili.

Mwamba ya kocha Peter Kephar ilitoka nyuma 0-7 na kupepeta Menengai Oilers ya kocha Gibson Weru 21-7 ugani Mombasa SC.

Nyota wa Kenya Shujaa, Daniel Taabu alifungia Mwamba mguso ulioandamana na mkwaju na kufanya pointi kuwa 7-7 baada ya Oilers kufungua ukurasa wa pointi kupitia mguso na mkwaju kutoka kwa Mark Kwemoi.

Taabu aliongeza mguso wa pili ambao pia ulikuwa na mkwaju na kuweka Mwamba kifua mbele 14-7 kabla ya Crispine Omondi kuzima kabisa Oilers na mguso wa mwisho. Taabu aliibuka mchezaji bora wa Driftwood Sevens.

Mwamba ni timu ya tatu msimu huu kushinda ligi hiyo ya duru sita. Mabingwa watetezi KCB walilaza Strathmore Leos 12-10 katika duru ya kwanza – Kabeberi Sevens – kabla ya Strathmore kulipiza kisasi katika fainali ya Christie Sevens kwa kulemea wanabenki hao 25-10. Duru mbili za kwanza zilifanyika uwanjani RFUEA jijini Nairobi. Duru zilizosalia ni Kakamega Sevens (Kakamega), Dala Sevens (Kisumu) na Prinsloo Sevens (Nakuru).

  • Tags

You can share this post!

Chama cha UDA chataka Babu Owino azimwe kushiriki uchaguzi...

Osano analenga Tuzo ya Mnyakaji Bora muhula ujao

T L