• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Mwanandondi Conjestina Achieng’ apata ajira kama mtumishi wa karibu wa Mike Sonko   

Mwanandondi Conjestina Achieng’ apata ajira kama mtumishi wa karibu wa Mike Sonko  

 

NA MERCY KOSKEI

NYOTA wa zamani wa ndondi Conjestina Achieng’, mnamo Ijumaa, Juni 16,2023, kwa mara ya kwanza aliripoti kazini tangu kuhitimisha muda wake katika kituo cha kurekebisha tabia na maadili (rehabilitation centre). 

Conjestina, bingwa wa Afrika mara mbili na mshindi wa zamani wa taji la dunia, aliandamana na gavana wa zamani wa Nairobi, Mike Sonko, hadi ofisini mwake Nairobi.

Sonko alimteua kama mkuu wa usalama, katika Salama Bling Beach Resort, Kanamai, Kaunti ya Kilifi.

Kupitia picha zilizosambazwa mitandaoni, siku yake ya kwanza kazini, Conjestina aliandamana na Sonko katika shughuli zake na alifanyiwa ziara ya ofisi kabla ya kutambulishwa kwa wafanyakazi wenzake.

Bingwa huyo wa michezo nchini alipigwa picha akimfungulia Sonko mlango wa gari, ikiashiria kuwa alikuwa mlinzi wake mkuu na wa karibu.

Pia alibeba mkoba wake, kazi ya kawaida ya walinzi wakuu, haswa wale wanaoshughulikia biashara za wafanyabiashara wakuu au wanasiasa.

Conjestina alimshukuru Bw Sonko kwa kujitokeza kumsaidia kupona kutokana na msongo wa mawazo baada ya kustaafu kucheza ndondi za kulipwa.

“Nimefurahi sana kuanza ukurasa huu mpya maishani mwangu na ninamshukuru Gavana Sonko kwa kunipa fursa hii. Nitajitahidi kumfanya ajivunie kazi yangu ,” Conjestina alisema Alhamisi, Juni 15, baada ya kukutana na Sonko.

Sonko alibainisha kuwa alikuwa na imani kuwa Conjestina angekuwa kiungo muhimu kwa timu yake kwani kwa sasa amepona kabisa.

“Conjestina ni nyota wa ndondi wa Kenya. Ni mfano wa kuigwa kwa vijana na ni mpiganaji. Nina imani kuwa atakuwa mtu muhimu kwa timu yetu,” Sonko alisema.

Sonko alikuwa amepanga kumwajiri Conjestina katika klabu yake ya usiku Mombasa, kabla ya kumhamisha kufanya kazi katika Salama Bling Beach Resort, Kanamai kama mwalimu wa mazoezi ya viungo na mkuu wa usalama.

 

 

  • Tags

You can share this post!

Poland waangusha Ujerumani katika pambano la kirafiki

Makahaba Thika wapandisha bei ya huduma, wakilalamikia...

T L