• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 5:01 PM
Poland waangusha Ujerumani katika pambano la kirafiki

Poland waangusha Ujerumani katika pambano la kirafiki

Na MASHIRIKA

BEKI Jakub Kiwior alifunga bao la pekee na la ushindi uliosajiliwa na Poland dhidi ya Ujerumani katika pambano lililompa kigogo Jakub Blaszczykowski fursa kuangika rasmi daluga zake kimataifa.

Blaszczykowski, 37, alichezea Poland mara 109, miaka minne baada ya mchuano wake wa awali ndani ya jezi za timu ya taifa na akaondoka uwanjani kwa heshima kubwa kutoka uwanjani baada ya dakika ya 16 inayoashiria nambari ya jezi yake.

Kiwior ambaye ni beki wa Arsenal, alicheka na nyavu za Ujerumani kunako dakika ya 31. Licha ya kuelekeza langoni makombora 26, Ujerumani hawakupata fursa ya kutikisa nyavu za Poland jijini Warsaw.

Ingawa walipewa penalti mwanzoni mwa kipindi cha kwanza kwa madai kuwa Jan Bednarek alikuwa amenawa mpira ndani ya kijisanduku, maamuzi hayo yalibatilishwa na teknolojia ya VAR.

Licha ya kupoteza mechi hiyo, Ujerumani bado wamefuzu kwa fainali za Euro 2024 kwa sababu watakuwa wenyeji wa kipute hicho. Hiyo ndio maana wanacheza mechi za kirafiki badala ya za kufuzu kwa kivumbi hicho.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wabunge waliokwepa kushiriki kura muhimu

Mwanandondi Conjestina Achieng’ apata ajira kama mtumishi...

T L