• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 8:50 AM
NYOTA WA WIKI: Karim Benzema

NYOTA WA WIKI: Karim Benzema

Na GEOFFREY ANENE

LICHA ya kugonga vichwa vya habari kwa sababu mbaya, Karim Benzema hajabururwa chini kimchezo na sakata hizo.

Yeye ni mmoja wa wafumaji matata wa magoli.

Mtoto huyo wa sita kutoka familia ya watoto tisa alianzia soka yake katika mtaa wake wa Bron Terraillon mjini Lyon akiwa na umri wa miaka minane.

Klabu ya Lyon ilivutiwa naye na kumnyakua alipoifunga mabao mawili katika mechi ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 10.

Alikuwa ‘ballboy’ wakati wa mechi za timu ya watu wazima ya Lyon na pia kuendelea kukuza uchezaji wake katika kikosi chake cha makinda.

Ripoti zinasema alifungia Lyon ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 magoli 38 katika ligi ya umri huo.

Alikuwa katika timu ya Ufaransa iliyotawala Kombe la Bara Ulaya la U17 mwaka 2004 mjini Chateauroux.

Aliingia katika kikosi cha kwanza cha Lyon wakati wa wachezaji Michael Essien, Florent Malouda, John Carew, Eric Abidal na Sylvian Wiltord mwaka 2005.

Alifungia Lyon mabao 66 katika michuano 148 katika mashindano yote kabla ya Real Madrid kumsaini Julai 2009.

Benzema amekamilisha misimu mitatu iliyopita akiwa mfungaji bora wa Real na wa pili kwenye La Liga nyuma ya nyota Lionel Messi aliyejiunga na Paris Saint-Germain kutoka Barcelona mwezi Agosti.

Benzema amechezea Real mechi 580 katika mashindano yote na kuifungia mabao 297 pamoja na kusuka pasi 181 zilizoishia kuwa magoli.

Anapokea mshahara wa Sh2.1 bilioni kila mwaka kambini mwa Real.

Benzema ameshinda Klabu Bingwa Ulaya mara nne, La Liga mara tatu na Klabu Bingwa Duniani mara nne.

Na Les Bleus, ameshinda Kombe la Uefa Nations League mwaka 2021.

Yeye ni mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Ufaransa mara tatu.

Anaaminika kuwahi kuchumbia mwanamuziki Mwamerika Rihanna kabla ya kuachana mwaka 2017.

El Gato ama Coco anavyofahamika kwa majina ya utani, alipata mtoto wa kike na Chloe de Launay, msichana Melia, mwaka 2014 na mtoto wa kiume mwaka 2017 na Cora Gauthier anayeitwa Ibrahim.

Anaaminika kuwahi kuchumbia mwanamuziki Mwamerika Rihanna.

  • Tags

You can share this post!

COVID-19: Vinara wa EPL wahimiza wachezaji kuchanjwa

UDAKU: Ya Balotelli na Messina yatibuka!

T L