Na MASHIRIKA
VINARA wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na Serikali ya Uingereza wamehimiza wanasoka kuchanjwa dhidi ya Covid-19.
Nusu ya mechi za EPL zilizokuwa zitandazwe wikendi hii tayari zimeahirishwa kutokana na ongezeko la maambukizi ya corona linalozidi kushuhudiwa katika klabu mbalimbali.
Katika ligi za daraja za pili, tatu na nne nchini Uingereza (EFL), asilimia 25 ya wachezaji tayari wamesema hawana nia ya kuchanjwa na tayari mechi 19 zilizokuwa zitandazwe Jumamosi ya Disemba 18, 2021 zimeahirishwa.
Kwa mujibu wa kocha Jurgen Klopp wa Liverpool, hatua ya wanasoka kuchanjwa ni dhihirisho la kiwango cha juu cha uwajibikaji. Mkufunzi huyo raia wa Ujerumani amefichua kwamba asilimia 99 ya kikosi chake kimepokea dozi mbili za chanjo.
Maoni sawa na yake yanashikiliwa pia na makocha Mikel Arteta na Pep Guardiola wa Manchester City.
Hali ilivyo katika Ligi Kuu za bara Ulaya:
Italia
Ufaransa
Ujerumani
Uhispania
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO