• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
UDAKU: Ya Balotelli na Messina yatibuka!

UDAKU: Ya Balotelli na Messina yatibuka!

IMEKUSANYWA NA CHRIS ADUNGO

HARUSI iliyokuwa ifanyike mwezi huu kati ya mshambuliaji wa zamani wa Manchester City na Liverpool, Mario Balotelli (juu pichani), na mwanamitindo Alessia Messina imeahirishwa.

Hii ni baada ya Balotelli, 31, kufichua kuwa mchumba wake huyo raia wa Italia ambaye pia ni mwanahabari, bado hajapata nafuu baada ya mimba kumharibikia Oktoba.

Awali, sogora huyo wa Italia ambaye sasa anachezea klabu ya Adana Demirspor nchini Uturuki, alikuwa amewataka mashabiki kujiandaa kwa sherehe kubwa ya ndovu kumla mwanawe Desemba 31.

Mpambe aliyetarajiwa kusimamia harusi hiyo ni kiungo matata wa Manchester United na timu ya taifa ya Ufaransa, Paul Pogba, anayetoka kwa sasa na kipusa Maria Zulay Salaues.

Balotelli alimvisha Messina, 28, pete ya uchumba Septemba mwaka jana baada ya kufahamiana kwa kipindi cha mwezi mmoja pekee.

“Ilikuwa iwe karamu kubwa licha ya corona. Mipango ilianza mapema lakini hali ya Messina si shwari,” akaandika Balotelli kwenye Instagram.

Hadi alipopata hifadhi ya penzi lake kwa Messina, Balotelli alikuwa ametoka kimapenzi na vidosho Dayane Mello, Fanny Neguesha na Katja Krasavice.

Messina, ambaye alikuwa mwaniaji wa taji la uanamitindo katika mashindano ya Big Brother, Temptation Island na Grande Fratello mnamo 2019, anajivunia zaidi ya wafuasi laki nane kwenye mitandao ya kijamii.

Hadi alipopata hifadhi ya penzi lake kwa Messina, Balotelli alikuwa ametoka kimapenzi na vidosho Dayane Mello, Fanny Neguesha na Katja Krasavice.

Kipusa Raffaella Fico alimzalia mtoto wa kike, Pia, mnamo 2012 kabla ya Clelia Carleenn kumzalia mtoto wa kiume kwa jina Lion mnamo 2017.

Balotelli alitemana na Clelia ambaye ni mwanabenki na mwanamitindo maarufu nchini Uswisi mwanzoni mwa 2019.

You can share this post!

NYOTA WA WIKI: Karim Benzema

Wanabodaboda Thika wahimizwa kuweka akiba kwa vikundi

T L