• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 5:04 PM
Real wazamisha Bilbao na kufungua mwanya kileleni mwa La Liga

Real wazamisha Bilbao na kufungua mwanya kileleni mwa La Liga

Na MASHIRIKA

KARIM Benzema alifunga mabao mawili na kusaidia Real Madrid kupepeta Athletic Bilbao 2-1 na hivyo kufungua mwanya wa alama nane kati yao na nambari mbili Sevilla kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga).

Mabao mawili ya haraka kutoka kwa nyota huyo raia wa Ufaransa yaliwapa Real uongozi wa 2-0 baada ya dakika saba za mwanzo wa kipindi cha kwanza. Benzema sasa anajivunia mabao 20 kapuni mwake msimu huu. Oihan Sancet alirejesha Bilbao mchezoni baada ya kuwafungia bao katika dakika ya 10.

Nico Williams na Inaki Williams walipoteza nafasi kadhaa za wazi za kusawazishia Bilbao katika kipindi cha pili licha ya kusalia uso kwa macho na kipa Thibaut Courtois. Kipa wa Bilbao, Julen Agirrezabala naye aliwanyima Eden Hazard na Toni Kroos nafasi za kufungia Real mabao zaidi mwishoni mwa kipindi cha pili.

Chini ya kocha Carlo Ancelotti, Real kwa sasa watasherehekea Krismasi wakiselelea kileleni mwa jedwali japo wametandaza mchuano mmoja zaidi kuliko washindani wao wakuu Sevilla. Real wamepoteza mechi mbili kati ya 25 kufikia sasa katika mashindano yote ya msimu huu.

Kichapo cha mwisho walichopokezwa kilikuwa dhidi ya Espanyol ligini mnamo Oktoba 3, 20

You can share this post!

Liverpool wadengua Leicester kwenye robo-fainali za Carabao...

Ramos aonyeshwa kadi nyekundu PSG wakikabwa koo na Lorient...

T L