• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 7:50 AM
Liverpool wadengua Leicester kwenye robo-fainali za Carabao Cup

Liverpool wadengua Leicester kwenye robo-fainali za Carabao Cup

Na MASHIRIKA

DIOGO Jota alifungia Liverpool penalti ya ushindi katika mechi iliyoshuhudia Liverpool wakitoka nyuma kwa mabao mawili na kutinga nusu-fainali za Carabao Cup kwa mara ya kwanza tangu 2017 baada ya kudengua Leicester City ugani Anfield.

Jota aliingia uwanjani katika kipindi cha pili matokeo yakiwa 3-1. Aliwafungia Liverpool bao la pili katika dakika ya 68 baada ya kukamilisha krosi ya Takumi Minamino aliyesawazisha mambo mwishoni mwa kipindi cha pili. Minamino alifanya mashindi wa mechi hiyo kuamuliwa kupitia mikwaju ya penalti alipovurumisha kimiani kombora kali kutokana na krosi ya James Milner aliyemtatiza sana kipa Kasper Schmeichel katika vipindi vyote viwili vya mchezo.

Minamino ambaye ni raia wa Japan, alipaisha mkwaju wake wa penalti baada ya kipa Caoimhin Kelleher kupangua mkwaju wa Luke Thomas. Hata hivyo, Ryan Bertrand alipoteza pia penalti yake kwa upande wa Leicester na hivyo kumpa Jota nafasi ya kufungia Liverpool mkwaju uliowavunia ushindi.

Liverpool sasa watakutana na Arsenal katika hatua ya nne-bora kwenye Carabao Cup msimu huu.

You can share this post!

Chelsea wasubiri hadi dakika za mwisho kubandua Brentford...

Real wazamisha Bilbao na kufungua mwanya kileleni mwa La...

T L