• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 5:55 AM
Sadio Mane afungua akaunti yake ya mabao kambini mwa Bayern Munich

Sadio Mane afungua akaunti yake ya mabao kambini mwa Bayern Munich

Na MASHIRIKA

SADIO Mane alifunga bao lake la kwanza akiwa mchezaji wa Bayern Munich mnamo Jumamosi usiku na kusaidia miamba hao wa Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) kupepeta RB Leipzig 5-3 katika pambano la kuwania taji la German Super Cup ugani Red Bull Arena.

Mane ambaye ni fowadi wa zamani wa Liverpool, alicheka na nyavu baada ya Jamal Musiala kufungulia Bayern ukurasa wa mabao. Magoli mengine ya Bayern yalijazwa kimiani na Benjamin Pavard, Serge Gnabry na Leroy Sane. Leipzig walifunga mabao yao kupitia kwa Marcel Halsterberg, Christopher Nkunku na Dani Olmo.

Bayern ambao wamekuwa wafalme wa Bundesliga kwa misimu 10 iliyopita, wamekuwa washiriki wa mara kwa mara wa kipute cha Super Cup ambacho hukutanisha wafalme wa Bundesliga na washikilizi wa taji la German Cup.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Leicester wakataa Sh5.7 bilioni ambazo Newcastle wametoa...

Uhuru aelezea manufaa ya Nairobi Expressway

T L