• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Salaalaa! Mwanamume aliyejisajili kama mwanamke mashindano ya chesi agunduliwa

Salaalaa! Mwanamume aliyejisajili kama mwanamke mashindano ya chesi agunduliwa

NA AREGE RUTH

MAAFISA wa mashindano ya chesi – Sataranji ya Kenya Open – yanayoendelea katika ukumbi wa Sarit Expo jijini Nairobi, wameshangazwa na tukio la mchezaji wa kiume kuwa miongoni mwa wachezaji wa kike katika mashindano hayo.

Kijana  huyo ambaye alijisajili kwa jina Millicent Awuor, aliibua mjadala baada ya kuwabwaga bingwa wa zamani wa Kitaifa wa Kenya Gloria Jumba (aliyekadiriwa 1487), na mchezaji bora wa Uganda Ampaira Shakira (1702).

Ushindi wake wa kushtukiza dhidi ya Jumba na Shakira ulisababisha kila mchezaji wa Kenya kujiuliza amekuwa wapi wakati wa mashindano mengine muhimu ya kitaifa ya Sataranji.

Mshindi wa kitengo cha Open atatia mfukoni Sh1 milioni. Ili kuficha utambulisho wake, kijana huyo ambaye jina lake halisi ni Stanley Omondi alifunika kichwa na uso kabisa kutumia hijab.

Alisema uamuzi wake wa kufanya udanganyifu katika mashindano hayo umechangiwa na zawadi ya fedha taslimu Sh500,000 kwa mshindi katika kitengo cha wanawake.

Tofauti na wachezaji wengine, hakuzungumza na mtu yeyote ikiwa ni pamoja na wapinzani wake.

  • Tags

You can share this post!

Mvua nyingi yafifisha msisimko wa Pasaka

Taita Taveta: Maafisa wachunguzwa kufuja Sh4m hafla ya Vita...

T L