• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Spark FC yacharaza Real Stars katika mojawapo ya matokeo mseto ya ligi

Spark FC yacharaza Real Stars katika mojawapo ya matokeo mseto ya ligi

Na PATRICK KILAVUKA

Spark FC iliiponda Real Stars 1-0 katika mojawapo ya matokeo mseto ya mechi za Ligi ya Kaunti ndogo ya FKF, Nairobi West uwanjani Kihumbuini.

Bao hilo ambalo lilizamisha matumaini Stars na kudumisha mchezo kuwa uhai lilipataikana dakika ya 40 kupitia Patrick Mutuku.

Kwenye ngarambe zingine, Lockdown iliizima Big Hawks 2-1. Mabao ya Lockdown yalifungwa na Patrick Moses na Kens Njuguna dakika ya 81 na 88 mtawalia ilhali la kufuta machozi la Hawks lilimiminiwa na Dennis Mzee dakika ya 76.

Kangemi Atletico iliiadhibu Royal Soccer  2-0 kupitia Fred Ouma na Moses Muia dakika ya 24 na 74 mtawalia.Kangemi PAG nayo iliandikisha sare ya 1-1 mbele ya Vintage FC.  PAG ilifunga kupitia Odondo Omollo dakika ya 57 ilhali Vintage ilitangulia dakika ya 17 kupitia David Avujwe.

  • Tags

You can share this post!

Mashine zapokonya wachunaji majanichai kazi

Corona: Kifo cha polisi chaanika mahangaiko