Na MASHIRIKA
TOTTENHAM Hotspur wanaoendelea kujisuka upya chini ya kocha Antonio Conte, wamejinasia huduma za Yves Bissouma kutoka Brighton kwa Sh3.7 bilioni.
Kiungo huyo raia wa Mali anakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Spurs baada ya kipa Fraser Forster na mfumaji Ivan Perisic.
Bissouma, 25, amewajibishwa na Brighton mara 124 tangu ajiunge nao kutoka Lille ya Ufaransa mnamo Julai 2018. Alitandaza mechi 26 za EPL mnamo 2021-22 na akafunga bao moja.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO