• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Spurs wasajili kiungo Bissouma kutoka Brighton

Spurs wasajili kiungo Bissouma kutoka Brighton

Na MASHIRIKA

TOTTENHAM Hotspur wanaoendelea kujisuka upya chini ya kocha Antonio Conte, wamejinasia huduma za Yves Bissouma kutoka Brighton kwa Sh3.7 bilioni.

Kiungo huyo raia wa Mali anakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Spurs baada ya kipa Fraser Forster na mfumaji Ivan Perisic.

Bissouma, 25, amewajibishwa na Brighton mara 124 tangu ajiunge nao kutoka Lille ya Ufaransa mnamo Julai 2018. Alitandaza mechi 26 za EPL mnamo 2021-22 na akafunga bao moja.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Ruto amkaripia Raila kufuatia vurugu zilizotokea Jacaranda

Malkia Strikers tayari kuelekea Brazil baada ya Mozzartbet...

T L