• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 9:55 AM
Swansea City na Bournmouth zashinda mkondo wa kwanza wa nusu-fainali za mchujo wa kufuzu EPL kwa msimu ujao wa 2021-22

Swansea City na Bournmouth zashinda mkondo wa kwanza wa nusu-fainali za mchujo wa kufuzu EPL kwa msimu ujao wa 2021-22

Na MASHIRIKA

SWANSEA City waliwakomoa Barnsley 1-0 katika mkondo wa kwanza wa nusu-fainali ya mchujo wa kufuzu kwa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Jumatatu usiku.

Bao la pekee katika mchuano huo lilipachikwa wavuni na fowadi mzoefu raia wa Ghana, Andre Ayew aliyemwacha hoi kipa Bradley Collins wa Barnsley katika dakika ya 39.

Swansea watawaalika Barnsley kwa mkondo wa pili uwanjani Liberty mnamo Mei 22 wakilenga ushindi au sare ya aina yoyote ili kutinga fainali itakayowakutanisha mshindi kati ya Brentford na AFC Bournemouth.

Bournemouth pia walijiweka sawa kufuzu kwa fainali kwenye mchujo huo wa kutafuta kikosi cha tatu baada ya Norwich City na Watford ambacho kitapanda ngazi kutoka Ligi ya Daraja la Kwanza (Championship) hadi EPL msimu ujao wa 2021-22.

Bournemouth waliteremshwa daraja hadi Championship mwishoni mwa msimu wa 2019-20 baada ya kunogesha kipute cha EPL kwa mihula mitano. Kikosi hicho kiliwachabanga Brentford 1-0 katika mkondo wa kwanza wa nusu-fainali mnamo Mei 17, 2021 uwanjani Vitality. Goli hilo la pekee na la ushindi lilijazwa kimiani na Danjuma Groeneveld katika dakika ya 55.

Fainali ya mchujo huo wa kufuzu kwa EPL au kusalia kwenye Championship itachezewa uwanjani Wembley, Uingereza mnamo Mei 29, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Zaidi ya Wakenya 700 wamezea mate nafasi nne za makamishna...

‘Lockdown’ ya Aprili 2021 ilivyoyumbisha biashara yake...