• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 3:16 PM
Thiago Silva sasa kuchezea Chelsea hadi Julai 2024

Thiago Silva sasa kuchezea Chelsea hadi Julai 2024

Na MASHIRIKA

BEKI mzoefu raia wa Brazil, Thiago Silva, ametia saini mkataba wa mwaka mmoja utakaomshuhudia sasa akichezea Chelsea hadi Juni 2024.

Silva alijiunga na Chelsea kutoka Paris Saint-Germain (PSG) mnamo 2020 na akasaidia kikosi hicho kunyanyua ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) katika msimu wake wa kwanza ugani Stamford Bridge.

Amechezea Chelsea jumla ya mechi 106 katika mashindano yote na kuongoza kikosi hicho kutinga fainali ya Carabao Cup mara moja na Kombe la FA mara mbili.

Silva, anayejivunia kuwajibikia Brazil mara 113, aliongoza miamba hao kutinga robo-fainali za Kombe la Dunia mnamo Disemba 2022 akiwa nahodha. Brazil ambao ni mabingwa mara tano wa Kombe la Dunia walidenguliwa na Croatia kupitia mikwaju ya penalti.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO 

  • Tags

You can share this post!

KCB, Kabras wabomoa wapinzani, Monks na Machine wakiduwaza...

Olivier Giroud abeba AC Milan dhidi ya Torino katika Ligi...

T L